Star Tv

Hali ya sintofahamu imezuka kwa wakazi wa kata ya Ruhembe wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro  kufuatia  watu 10 wakazi wa kata  hiyo kupotea kwa siku 18 mara baada ya watu hao  kudaiwa kwenda kufanya shughuli za kibinadamu  katika hifadhi ya taifa ya Mikumi kinyume cha sheria na kupotelea huko mpaka sasa .

Tukio hilo la kupotea kwa watu hao 10 limetajwa kutokea Aprili mbili mwaka huu  majira ya asubuhi mara baada ya watu hao kuaga kuwa wanakwenda shambani  na kisha kuingia kwenye hifadhi ya taifa ya Mikumi kwa ajili ya kufanya shuguli mbalimbali za kibinadamu  na baada ya hapo watu hao wakashindwa kurejea kijijini  hatua iliyopelekea wananchi kuwa na mashaka na watu hao kutokana na  siku kusonga mbele bila watu hao kurejeaa kijijini akibainishandiwani wa kata hiyo Salim Mponzi na mwenyekiti wa kijiji hicho Mohamed Kapyale.

Kufuatia tukio hilo imemlazimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la Polisi Wilbroad Mutafungwa kufika katika kijiji hicho na kuongea na wananchi  kuhusu kutokea kwa tukio hilo huku akiwaomba wananchi hao kutoa ushirikiano kwa Jeshi la polisi ili kuweza kubaini mahali walipo watu hao  .

 

 Licha ya watu hao kupotea  katika hifadhi ya Mikumi, watu wengine wanaoishi kijijini hapo wameendelea  kufanya shughuli zao ndani ya hifadhi hiyo  bila kuhofia chochote hatua inayomshangaza kamanda Mutafungwa huku uongozi wa kijiji ukiwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi. 

Hata hivyo kamanda Mutafungwa amekemea tabia ya baadhi ya wananchi wanaopakana na hifadhi za taifa kufanya shughuli mbalimbali  za kibinadamu ndani ya hifadhi hizo bila ya kuwa na kibali. 

Jitihida za kuwatafuta watu hao  bado  zinaendelea kufanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana  na askari wa wanyama pori kutoka katika hifadhi ya Mikumi ili kujua kipi kimewapata watu hao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.