Star Tv

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mikutano ya kipupwe(Spring Meetings)  ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) inayofanyika mjini Washington DC, Marekani.

Akizungumza kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania Mjini Washigton DC, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amesema kuwa ujumbe wa Tanzania unaojumuisha pia wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi-Zanzibar, utasimamia maslahi ya pande zote mbili za Muungano.

Mikutano hiyo inatoa fursa kwa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu kutoka katika nchi wanachama ambao pia mi Magavana wa Benki ya Dunia na IMF, kujadili maendeleo na changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika utekelezaji wa masuala mbalimbali ya maendeleo na ushirikiano.

Aidha Mikutano hiyo hutoa fursa kwa nchi kushiriki kama mwanahisa kwenye mikutano ya kiutawala (Board of Governors) ya Taasisi hizo mbili ambapo maamuzi ya kiuendeshaji na kisera hufanyika

Tanzania itapata fursa ya kushiriki kwenye Kamati Maalum za Benki ya Dunia na IMF na baadhi ya mikutano hiyo ni Mkutano wa Mawaziri wa Fedha inayoshughulikia sera na utulivu wa Sekta ya fedha (International Monetary Committee and Finance Committee-IMFC

Dkt. Mpango atashiriki katika majadiliano na viongozi wa juu wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF wanaoshughulikia masuala ya Afrika kuhusu utekelezaji wa program za sera za kiuchumi, mikopo nafuu na misaada ya kitaalam kwa Tanzania

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.