.
Watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa kufuatia majibizano ya risasi baina yao na polisi wakati wakiwapeleka askari hao ili kuwaonesha katika eneo la maficho mahala ambapowalikuwa wakitunzia silaha mbalimbali walizokuwa wakizitumia katika matukio kadhaa ya uhalifu katika eneo la Kiraka Cheusi nje kidogo ya barabara kuu ya Nyakanazi- Rusumo wilayani Biharamulo mkoani Kagera.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera kamishina msaidizi wa polisi Revocatus Malimi amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa majibizano hayo yametokea wakati majambazi hao waliokuwa tayari chini ya ulinzi kutakiwa kuonesha maficho ya silaha waliyokuwa wakiitumia inayodaiwa kuhifadhiwa katika eneo hilo la pori lijulikanalo kama Kiraka Cheusi.
Kamanda Malimi amesema mara baada ya kukamatwa kwa majambazi katika eneo hilo la Kiraka Cheusi waliojulikana kwa majina ya Shaban Mangote mwenye umri wa miaka 40 na Erick Samson mwenye umri wa miaka 19, huku mmoja ambaye hakuweza kutambulika wote hao walikuwa wanatafutwa kwa kujihusisha na matukio ya utekaji magari na unyang’a nyi wa kutumia silaha katika eneo hilo la kiraka cheusi na ngazi saba wilayani Biharamulo.
Aidha kamanda Malimi ametoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo vya uhalifu kuacha mara moja na kuwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo endapo watakuwa na mashaka juu ya mtu asiye fahamika.