Star Tv

.

Watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa kufuatia majibizano ya risasi baina yao na polisi   wakati wakiwapeleka askari hao ili kuwaonesha katika eneo  la maficho mahala ambapowalikuwa wakitunzia silaha mbalimbali walizokuwa wakizitumia katika matukio kadhaa ya uhalifu  katika eneo la Kiraka Cheusi nje kidogo ya barabara  kuu ya Nyakanazi- Rusumo wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

 

Kamanda wa polisi  mkoa wa Kagera  kamishina msaidizi wa polisi Revocatus  Malimi amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa majibizano hayo yametokea wakati majambazi hao waliokuwa tayari chini ya ulinzi kutakiwa kuonesha maficho ya silaha waliyokuwa wakiitumia inayodaiwa kuhifadhiwa katika   eneo hilo la pori lijulikanalo kama Kiraka Cheusi.

Kamanda Malimi amesema mara baada ya kukamatwa kwa majambazi  katika eneo hilo la Kiraka Cheusi   waliojulikana kwa majina ya Shaban Mangote  mwenye umri wa miaka 40   na Erick Samson mwenye umri wa miaka 19, huku mmoja ambaye hakuweza kutambulika  wote hao walikuwa wanatafutwa kwa kujihusisha na matukio ya utekaji magari na unyang’a nyi wa kutumia silaha katika eneo hilo la kiraka cheusi na ngazi saba wilayani Biharamulo.

Aidha kamanda  Malimi ametoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo vya uhalifu kuacha mara moja na kuwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo endapo watakuwa na mashaka juu ya mtu asiye fahamika.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.