Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF profesa Ibrahim Lipumba ametoa wito kwa wanachama wa chama hicho kuendelea kuunga mkono CUF kwasababu wamekijenga kwa muda mrefu kwa kudai haki katika nyanja mbalimbali ikiwemo demokrasia ya kweli na kupata katiba mpya.
Profesa Lipumba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimio ya mkutano mkuu uliyofanyika wiki iliyopita.
Amewataka wanachama wa chama wanaohama chama hicho kutofanya vitendo vya kijinai kwa kuchoma moto bendera ya CUF pamoja na kubadilisha rangi ya ofisi za chama hicho.