Star Tv

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe ameshauri vyombo vya kutoa haki viweke mikakati ya namna ya

kupunguza mahabusu, akidai kwamba vyombo hivyo kama vitapitia vizuri makosa ya mahabusu hao, itagundua kuwa nusu ya wafungwa walioko

magerezani hawakustahili kuwepo huko. 

 

Mbowe amesema, amekutana na mambo ya kuumiza alipokuwa mahabusu katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam, tangu Novemba 2018 Mbowe

ametoa kauli hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, kuhusu kuondoka kwa Edward Lowassa Mbowe amemtaka kusema ukweli huko aliko na kwamba kukihama chama hicho yalikuwa ni maamuzi yake binafsi. Katika hatua nyingine Kiongozi huyo wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni amemwagiza aliyekuwa mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kuzungumza kile kilichotokea hadi kuvuliwa ubunge. Mbowe amesema halengi kumtetea Nassari lakini amemwagiza kuzungumza na wananchi wa jimbo lake na wanachama juu ya kipi kimetokea. Huku  Mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko kwa upande wake amesema hajutii kukaa Segerea kwa sababu amejifunza mengi na ameona mengi,

Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko wamekaa kwa zaidi ya miezi mitatu gerezani kutokana na kosa la kukiuka masharti ya dhamana.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.