Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe ameshauri vyombo vya kutoa haki viweke mikakati ya namna ya
kupunguza mahabusu, akidai kwamba vyombo hivyo kama vitapitia vizuri makosa ya mahabusu hao, itagundua kuwa nusu ya wafungwa walioko
magerezani hawakustahili kuwepo huko.
Mbowe amesema, amekutana na mambo ya kuumiza alipokuwa mahabusu katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam, tangu Novemba 2018 Mbowe
ametoa kauli hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, kuhusu kuondoka kwa Edward Lowassa Mbowe amemtaka kusema ukweli huko aliko na kwamba kukihama chama hicho yalikuwa ni maamuzi yake binafsi. Katika hatua nyingine Kiongozi huyo wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni amemwagiza aliyekuwa mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kuzungumza kile kilichotokea hadi kuvuliwa ubunge. Mbowe amesema halengi kumtetea Nassari lakini amemwagiza kuzungumza na wananchi wa jimbo lake na wanachama juu ya kipi kimetokea. Huku Mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko kwa upande wake amesema hajutii kukaa Segerea kwa sababu amejifunza mengi na ameona mengi,
Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko wamekaa kwa zaidi ya miezi mitatu gerezani kutokana na kosa la kukiuka masharti ya dhamana.