Fuvu la kichwa na mabaki ya mwili wa mwanafunzi Alex Pastory wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Nyugwa wilayani Nyang’hwale mkoani Geita kimekutwa kwenye shamba la mwananchi mmoja sababu za kifo chake zikiwa bado hazijafahamika.
Hayo yamezungumzwa na Kamanda wa Polisi Mkoani Geita Mponjoli Mwabulambo wakati akiongea na Waandishi wa habari, ambapo amesema marehemu wakati akiwa shuleni akiendelea na masomo kuna wakati aliomba ruhusa ya kwenda Nyumbani kwao ukelewe kwa madai ya kwenda kutibiwa na kutokana na hali yake ya afya kurejea alirudi shule Februari 28 mwaka huu na kuendelea na masomo.
Na kwamba tangu tarehe 1 mwezi Machi alitoweka shuleni na sehemu ambayo alikuwa anaishi kwa kupanga hakuonekana kwani nyumbani kwao ni Ukerewe na ilipofika tarehe 8 mwezi huu kuna mwanamke alikuwa akilima shambani ndipo alipoona fuvu la Binadamu huku jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hili ili kujua chanzo cha kifo chake. Hayo yakisemwa na SACP Mponjoli Mwabulambo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita