Star Tv

Fuvu la kichwa na mabaki ya mwili wa mwanafunzi Alex Pastory wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Nyugwa wilayani Nyang’hwale mkoani Geita kimekutwa kwenye shamba la mwananchi mmoja sababu za kifo chake zikiwa bado hazijafahamika.

 

Hayo yamezungumzwa na Kamanda wa Polisi Mkoani Geita Mponjoli Mwabulambo wakati akiongea na  Waandishi wa  habari, ambapo amesema marehemu wakati akiwa shuleni akiendelea na masomo kuna wakati aliomba ruhusa ya kwenda Nyumbani kwao ukelewe kwa madai ya kwenda kutibiwa na kutokana na hali yake ya afya kurejea  alirudi shule Februari 28  mwaka huu na kuendelea na masomo.

 

Na kwamba  tangu tarehe 1 mwezi Machi  alitoweka shuleni  na sehemu ambayo alikuwa anaishi kwa kupanga hakuonekana kwani nyumbani kwao ni  Ukerewe  na ilipofika tarehe 8 mwezi huu kuna mwanamke alikuwa akilima shambani ndipo alipoona fuvu la Binadamu huku jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hili ili kujua chanzo cha kifo chake. Hayo yakisemwa na SACP Mponjoli Mwabulambo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.