MWANAMKE mmoja aliyejulikana kwa jina la Magreth Sinkamba mkazi wa kijiji cha Mpui Wilaya ya Momba Mkoani Songwe anashikiliwa na Jeshi la polisi kwa tuhuma za kumuua Mumewe kwa kipigo....
Imezoeleka katika jamii wanawake ndio wamekuwa wakipigwa na waume zao ama na wanaume kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ugomvi wa kifamilia na wivu wa kimapenzi, lakini katika tukio hili hali ni tofauti mwanamke amempiga Mumewe na kusababisha kifo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Kamishna msaidizi wa Polisi Mathias Nyange amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Matukio ya namna hiyo yamekuwa yakitokea lakini kuna usiri kwa wanaume kujitokeza Nyange anatoa Wito kwa Wanaume sasa kuvunja Ukimya pale wanapokutwa na maswahibu hayo.