Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za serikali za msingi na sekondari na amewaagiza mawaziri wenye dhamana kushugulikia agizo hili mara moja.
Rais Magufuli amebainisha hayo wakati wa kikao cha pamoja na Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani S. Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce L. Ndalichako Ikulu jijini Dar es salaam.