Star Tv

January 15, 2018 Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ametoa taarifa inayoelezea mambo aliyoyajadili wakati alipokwenda IKULU kukutana na Rais Magufuli January 9 2018.

Baada ya kutoka IKULU hiyo January 9 Lowassa alisifia utendaji kazi wa Rais Magufuli kwa aliyoyafanya toka ameingia madarakani ambapo alitaka pia Watanzania waendelee kumuunga mkono.

Taarifa ya Lowassa ya leo inanukuliwa ikiwa imeandikwa yafuatayo

 “Mnamo January 9 2018 nilipokea mwaliko kutoka kwa Rais Dr. John Pombe Magufuli akiniomba kwenda kukutana nae IKULU siku hiyohiyo kwa ajili ya mazungumzo“

Aidha, Jumapili January 14 2018 nilipata fursa ya kukielezea kwa kina Chama changu kupitia kikao cha kamati kuu ya mazungumzo yangu na Rais Dr. Magufuli IKULU, ujumbe wa Rais Magufuli kwangu ulikua ni kunishawishi nirejee CCM suala ambalo sikukubaliana nalo

Na nilimueleza Rais ya kwamba uamuzi wangu wa kukihama chama hicho na kujiunga CHADEMA haukuwa wa kubahatisha” – Edward Lowassa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.