Star Tv

Msako wa madawa ya kulelya kwa kutumia kikosi cha mbwa maalum wa Polisi wenye mafunzo ya kijeshi umeanza kuzaa matunda mkoani Singida, baada ya kufanikiwa kukamata viroba vya bangi iliyokuwa ikisafirishwa kwa basi kutoka Kahama-Shinyanga kwenda Jijini Dar-es-salaam.

Ilikuwa mapema asubuhi katika eneo la mzani barabara kuu ya Singida- Mwanza, wakati zoezi la ukaguzi wa magari mbalimbali lilipoanza ili kusaka madawa ya kulelya kwa kutumia kikosi cha mbwa wa Jeshi la Polisi wenye mafunzo maalum kwa ajili ya kufanya shughuli hiyo muhimu.

Hata hivyo baadaye jioni Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Isaya Mbughi, akakutana na waandishi wa habari na kutoa taarifa za kufanikiwa kukamata viroba vya bangi kwenye basi la abiria.

Kaimu Kamanda Mbughi anasema ingawa mwenye bangi hiyo anadaiwa kupanda gari lingine, lakini polisi wanaendelea kuwashikilia mafundi wawili wa basi hilo ambao walikabidhiwa mzigo huo.

Wakati mwenye bangi bado anaendelea kutafutwa, mafundi wa basi waliokabidhiwa mzigo huo toka Kahama wanatarajiwa kupandishwa kizimbani wakati kwa ajili ya kujibu shitaka linalokabili.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.