Msako wa madawa ya kulelya kwa kutumia kikosi cha mbwa maalum wa Polisi wenye mafunzo ya kijeshi umeanza kuzaa matunda mkoani Singida, baada ya kufanikiwa kukamata viroba vya bangi iliyokuwa ikisafirishwa kwa basi kutoka Kahama-Shinyanga kwenda Jijini Dar-es-salaam.
Ilikuwa mapema asubuhi katika eneo la mzani barabara kuu ya Singida- Mwanza, wakati zoezi la ukaguzi wa magari mbalimbali lilipoanza ili kusaka madawa ya kulelya kwa kutumia kikosi cha mbwa wa Jeshi la Polisi wenye mafunzo maalum kwa ajili ya kufanya shughuli hiyo muhimu.
Hata hivyo baadaye jioni Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Isaya Mbughi, akakutana na waandishi wa habari na kutoa taarifa za kufanikiwa kukamata viroba vya bangi kwenye basi la abiria.
Kaimu Kamanda Mbughi anasema ingawa mwenye bangi hiyo anadaiwa kupanda gari lingine, lakini polisi wanaendelea kuwashikilia mafundi wawili wa basi hilo ambao walikabidhiwa mzigo huo.
Wakati mwenye bangi bado anaendelea kutafutwa, mafundi wa basi waliokabidhiwa mzigo huo toka Kahama wanatarajiwa kupandishwa kizimbani wakati kwa ajili ya kujibu shitaka linalokabili.
Picha na mtandao.