Star Tv

Wakili wa utetezi katika kesi ya utakatishaji fedha inayomkabili aliyekuwa Rais wa (TFF) Jamal Malinzi na wenzake ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuamuru upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hayo yameelezwa na wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leonard Swai kueleza upelelezi haujakamilika.

Swai amedai kuwa kesi ya Malinzi na wenzake imeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika, hivyo anaomba iahirishwe. Kutokana na hatua hiyo, Wakili Nkoko amedai kuwa kesi hiyo imechukua muda mrefu na kila siku wanaambiwa jalada bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Ameeleza kuwa ni miezi miwili imepita sasa anaiomba mahakama itumie uwezo wake kuiharakisha kesi hiyo ili iweze kuanza kusikilizwa na kuendelea kuwa upande wa mashtaka umewafungulia washtakiwa kesi ya utakatishaji ili kuwakomoa hivyo wanatumia kesi hiyo kama ngao ya ukandamizaji.

Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mashauri amesema mahakama hiyo inafanya kazi ya kutafsiri sheria na kama itafanya vinginevyo itakuwa nje ya sheria. Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi January 11, 2018.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.