Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo amewaongoza watanzania katika kutoa salamu za mwisho kwa watu 19, waliopoteza maisha kutokana na ajali iliyosababishwa na kudondoka kwa ndege katika mkoa wa Kagera wilayani Bukoba.
Salamu hizo za mwisho zimetolewa katika uwanja wa Kaitaba Wilayani Bukoba. Huku katika ajali hiyo watu 24 walinusurika na kuweza kuokolewa kutoka katika ndege hiyo ambayo ni mali ya kampuni ya usafirishaji ya Precision.Ndege hiyo iliyokuwa ikifanya safari zake kutokea Dar –es-salaam kuja Bukoba baada ya kuanguka ndani ya ziwa Viktoria kando na uwanja wa ndege wa Bukoba. Ajali hiyo ya ndege ilitokea majira ya saa mbili na nusu asubuhi tarehe 06/11, wakati ikitaka kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba. Huku serikali ikiahidi kugharamia mazishi ya waliopoteza maisha.