Star Tv

Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo amewaongoza watanzania katika kutoa salamu za mwisho kwa watu 19, waliopoteza maisha kutokana na ajali iliyosababishwa na kudondoka kwa ndege katika mkoa wa Kagera wilayani Bukoba.

Salamu hizo za mwisho zimetolewa katika uwanja wa Kaitaba Wilayani Bukoba. Huku katika ajali hiyo watu 24 walinusurika na kuweza kuokolewa kutoka katika ndege hiyo ambayo ni mali ya kampuni ya usafirishaji ya Precision.Ndege hiyo iliyokuwa ikifanya safari zake kutokea Dar –es-salaam kuja Bukoba baada ya kuanguka ndani ya ziwa Viktoria kando na uwanja wa ndege wa Bukoba. Ajali hiyo ya ndege ilitokea majira ya saa mbili na nusu asubuhi tarehe 06/11, wakati ikitaka kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba. Huku serikali ikiahidi kugharamia mazishi ya waliopoteza maisha.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.