Star Tv

Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo amewaongoza watanzania katika kutoa salamu za mwisho kwa watu 19, waliopoteza maisha kutokana na ajali iliyosababishwa na kudondoka kwa ndege katika mkoa wa Kagera wilayani Bukoba.

Salamu hizo za mwisho zimetolewa katika uwanja wa Kaitaba Wilayani Bukoba. Huku katika ajali hiyo watu 24 walinusurika na kuweza kuokolewa kutoka katika ndege hiyo ambayo ni mali ya kampuni ya usafirishaji ya Precision.Ndege hiyo iliyokuwa ikifanya safari zake kutokea Dar –es-salaam kuja Bukoba baada ya kuanguka ndani ya ziwa Viktoria kando na uwanja wa ndege wa Bukoba. Ajali hiyo ya ndege ilitokea majira ya saa mbili na nusu asubuhi tarehe 06/11, wakati ikitaka kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba. Huku serikali ikiahidi kugharamia mazishi ya waliopoteza maisha.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.