Star Tv

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Bora na Serikali za mitaa (USEMI) ikiongozwa na Jaffari Chaurembo, Mbunge wa Jimbo la Mbagala haijaridhishwa na kasi ya Ujenzi wa Shule mpya maalum ya Sekondari ya Bweni na sayansi ya Wasichana katika Mkoa Kagera kupitia Mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP).

Hayo yamebainishwa leo Oktoba 25, 2022 wakati Kamati hiyo ya USEMI ikipokea na kujadili taarifa kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa shule mpya 10 za wasichana zinazojengwa katika mikoa 10 ya awali ambapo kila mkoa utajengewa shule moja.

“Leo tumepokea taarifa za ujenzi wa shule mpya katika mikoa 10, Wapo waliofikia asilimia 80 lakini Kamati imesikitishwa sana na Mkoa Kagera, ujenzi unaenda taratibu mno na bado wapo chini ya asilimia ambayo tuliitarajia”-Chaurembo.

Kwa Upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Angellah Kairuki amesema Serikali ilitoa Bilioni 3 kwa kila mkoa katika Mikoa 10 na ikaagiza kufikia tarehe 31 Disemba 2022 Ujenzi wa madarasa na miundombinu yote iwe imekamilika kwa viwango kulingana na miongozo iliyowekwa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.