Star Tv

Watu wawili wamefariki Dunia na wengine ambao idadi kamili bado haijafahamika wamejeruhiwa baada ya kuibuka vurugu kati ya Askari Polisi na wakazi wa Kijiji cha Ikwambi kata ya Mofu wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro.

Kwa mujibu wa Mkuu wa mkoa wa Morogoro Fatma Mwasa amesema chanzo ni wakulima ambao ni wakazi wa kijiji hicho kuwafungia ndani ya ofisi ya Kijiji wenyeviti wa vitongoji, vijiji pamoja na Wafugaji kwa lengo la kutaka kuwachoma Moto wakiwatuhumu kushindwa kuwasaidia pindi wafugaji wanapoingiza mifugo katika mashamba yao.

Aidha watu wawili hao waliofariki ni Wakulima (mwanamke na mwanaume).

Miongoni mwa waliojeruhiwa ni Diwani wa kata hiyo Greyson Mgonela, ambaye baada ya kufanya mazungumzo naye kwa njia ya simu amesema wakati vurugu zinatokea wananchi walikuwa wakitumia silaha za jadi, Mawe, Mikuki na Marungu kuwapiga Askari, huku Askari nao wakitumia Mabomu ya Machozi na Kisha Risasi za Moto.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.