Star Tv

Siku moja baada ya aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kutangaza kujiuzulu, Bunge limetangaza kusitisha shughuli zake zote mpaka atakapopatikana spika mpya Februari mosi mwaka huu.

Katika taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Januari 7, 2022 na Katibu wa bunge, Nenelwa Mwihambi imesema taratibu za uchaguzi wa kujaza nafasi ya Spika zinaendelea huku akitangaza kuahirishwa vikao vya Kamati za Bunge ambavyo vilipangwa kuanza wiki ijayo.

Kwa mujibu wa tangazo la katibu huyo wa Bunge kwa wabunge, amesema hakuna shughuli zitakazoendelea kwa kipindi ambacho nafasi ya Spika iko wazi hivyo amewaagiza wabunge wote kufika jijini Dodoma Januari 31, 2022 kwa ajili ya kuanza Mkutano we Sita wa Bunge utakaoanza Februari Mosi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.