Star Tv

Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Ashatu Kachambwa Kijaji aliyefika Ikulu, Zanzibar kujitambulisha rasmi.

Rais amempongeza Waziri Dkt. Kijaji kwa kuendeleza ushirikiano kati ya Wizara hiyo na Wizara ya Ujenzi na Mawasiliano ya Zanzibar, Ambapo ametaka uhusiano uendelee kuwa imara mara zote kwa maslahi mapana ya taifa.

Aidha Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza haja ya kuendelezwa ushirikiano kati ya Wizara mbili hizo na kusema ana matumaini makubwa mafanikio zaidi yataendelea kupatikana kwa azma ile ile ya kuiletea maendeleo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wake Waziri Dkt. Ashatu Kijaji aliyeongozana na ujumbe wa Wizara yake akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula amemshukuru Rais Mwinyi na kuahidi kufanyia kazi maelekezo na ushauri alioutoa kwa maslahi mapana ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.