Star Tv

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amewakaribisha Wawekezaji kutoka Jamhuri ya Kiarabu ya Misri kuwekeza na kufanya biashara na Tanzania kutokana na uwepo wa mazingira rafiki na fursa za uwekezaji.

Waziri nchemba ametoa rai hiyo mjini Cairo Misri, wakati wa Kongamano la Kimataifa la Ushirikiano la Misri (Egypt International Cooperation Forum) lililowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo washirika wa maendeleo kutoka Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika, Benki ya Ulaya, Jumuiya ya Ushirikiano wa Uchumi na Maendeleo, Sekta Binafsi na Asasi za Kiraia.

Dkt. Mwigulu alisema kuwa kuna umuhimu wa kusisitiza kukuza mahusiano ya kimataifa hususan kwa nchi za kiafrika zinazoendelea na kuweka mikakati endelevu ya kupambana na athari za janga la UVIKO – 19, ili kukuza uchumi.

“Katika Kongamano hili tumejadilia namna bora ya kusaidiana katika mitaji hususani katika nchi zenye Taasisi za Kifedha zenye uwezo wakutoa fedha katika mazingira ya UVIKO-19 kutokana kuathiri shughuli nyingi za kiuchumi”, alieleza Dkt. Nchemba.

Aidha Dkt. Nchemba ameipongeza Wizara ya Ushirikiano ya Kimataifa ya Jamhuri ya Kiarabu ya Misri kwa kuandaa kongamano hilo kwa kuwa limeunganisha wadau kutoka sehemu mbalimbali duniani na kutoa fursa ya kuweza kujadiliana na kupeana uzoefu kwa lengo la kuleta maendeleo.

Kongamano la Kimataifa la Ushirikiano la Misri (Egypt International Cooperation Forum) linalofanyika kwa siku 2 limehudhuriwa na nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania, Malawi, Senegal, Kenya, Namibia na Zambia.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.