Mahakama ya hakimu Mkazi mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro imeamuru kufukuliwa kwa Kaburi palipozikwa mwili wa mtu mmoja.......
Mahakama ya hakimu Mkazi mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro imeamuru kufukuliwa kwa Kaburi palipozikwa mwili wa mtu mmoja aliyekutwa akiwa amefariki dunia katika Mto Ghona ulio Karibu na shule ya sekondar Scolastica ili ufanyiwe vipimo vya uchunguzi ili kubaini kama ni mwili wa Mwanafunzi Humphrey Makundi aliyekuwa anasoma shule ya sekondari Scolastica baada ya kutoweka shuleni hapo tangu Novemba 07 mwaka huu bila taarifa zozote.Mwili huo ulizikwa na Manispaa ya Moshi Novemba 12 mwaka huu baada ya kile kilichodaiwa kukosekana kwa ndugu na jamaa wa kutambua mwili huo ambayo ulihifadhiwa katika hospitality ya Mkoa ya Mawenzi iliyopo mjini moshi
Zoezi hili linafanyika muda huu katika makaburi ya Karanga yaliyopo katika Manispaa ya Moshi.
Picha na mtandao.