Star Tv

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezipiga faini ya Shilingi Bilioni 38.1 kampuni sita za simu kwa kosa la kutofikia viwango vya ubora wa huduma kama ilivyoanishwa na kanuni za ubora wa huduma za mwaka 2018.

Mamlaka hiyo kupitia Mkurugenzi wa TCRA, James Kilaba amezielekeza kampuni hizo kutozipeleka fedha hizo TCRA badala yake wazitumie katika kuwekeza kuboresha ubora wa huduma ndani ya siku 90.

Kampuni hizo na faini zilizotozwa kwenye mabano ni Airtel (Sh. Bilioni 11.5), Tigo (Sh. Bilioni 13), Halotel (Sh. Bilioni 3.4), Vodacom (Sh. Bilioni 7.8), Zantel (Sh. Bilioni 1) na TTCL (Sh. Bilioni 1.3).

Mkurugenzi wa TCRA, James Kilaba amesema mamlaka hiyo ilipima ubora wa huduma za mawasiliano katika robo ya mwisho wa mwaka 2020 na kubaini watoa huduma hao hawakufikia baadhi ya vigezo vya viwango vya ubora.

Amesema kwa mujibu wa kanuni ya 20 ya kanuni za ubora wa huduma za mawasiliano, mtoa huduma anayeshindwa kufikia vigezo anatakiwa kulipa faini.

“TCRA imeazimia kwamba badala ya kulipwa fedha hizo, tuzielekeze kwa watoa huduma. Kila mtoa huduma atumie kiasi chake alichotakiwa kulipa, akiwekeze katika kuboresha huduma”-

Aidha, Kilaba amesema anatoa siku tisini kwa kampuni hizo kutimiza makubaliano ya faini hiyo kwani wamekubaliana kwa kusaini hati ya makubaliano maalum, na ikiwa kuna mtoa huduma atakayefanya kinyume, TCRA itachukua hatua zaidi za kiudhibiti na kisheria pasipo kutoa taarifa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.