Uchache wa madarasa, utoro wa wanafunzi na walimu unadaiwa kuwa chanzo cha wanafunzi kufeli masomo yao wakati muunganiko wa ushirikiano baina ya wazazi na walimu ukiongeza nafasi ya kufeli kwa wanafunzi na kutojua kusoma kwa asilimia 28 nchi nzima.
Wanafunzi wanasema kuwa kubanana madarasani ndiko kunasabaisha baadhi ya wanafunzi kufika mpaka darasa la saba kuto jua kusoma. Inadaiwa kuwa kuwekwa nguvu kubwa katika madarasa ya saba na nne ndio huenda kikawa chanzo cha wanafunzi wengi kuhitimu elimu ya msingi wakiwa jui kusoma.
Halmshauri ya Mji wa Njombe inadaiwa kuwa ina asilimia 55 ya wanafunzi wanao jua kusoma na wamepita darasa la pili, wakati asilimia zinazo baki ni wale ambao hawajuu kusoma na kufanya hesabu za darasa la pili kwa mujibu wa utafiti wa Twaweza mwaka 2015.
Utafiti huo umefanyika nchi nzima na kubaini mapungufu mabilimbali na hakuna waliyo tafiti na kufika asilimia 100, hasa serikali ikiwa inatoa elimu bila malipo kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.
Picha na mtandao.