Star Tv

Rais wa John Pombe Magufuli amempongeza mwanasiasa wa upinzani Maalim Seif Shariff kwa kukubali kujiunga na Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) visiwani Zanzibar.

Rais Magufuli amesema kuwa uamuzi huo wa Maalim Seif ulikuwa ni wa busara na ulioangalia maslahi ya Zanzibar.

"Uliacha maslahi yako binafsi, ukafanya uamuzi mkubwa na wa busara kwa maslahi ya Wazanzibari," ameeleza Magufuli na kuongeza: "Kuna ndoa zilivunjika, hasa Pemba kutokana na uchaguzi kwa kuwa mwanamke kapigia kura CCM na mume ACT, lakini baada ya maamuzi ya Maalim Seif wanandoa hao wakarudiana."-Rais Magufuli.

Mwezi Desemba ACT ilitangaza kukubali kuingia katika serikali ya Zanzibar kama katiba ya visiwa hivyo inavyoelekeza na kupendekeza jina la Maalim Seif kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, Maamuzi ambayo yalipokelewa kwa hisia mseto huku baadhi ya wanaharakati wakikikosoa chama hicho kwa 'kuwasaliti wananchi.

Rais Mwinyi na Maalim Seif wapo nyumbani kwa rais Magufuli wilayani Chato kwa ziara ya siku mbili.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.