Star Tv

Viongozi wa bodi katika vituo vya afya wilayani Tarime mkoani Mara wameonywa kuacha tabia ya kununua dawa za binadamu katika maduka ya nchi jirani ya Kenya badala yake watumie ya hapa nchini yaliyoidhinishwa na serikali.

Ni katika kikao cha kuunda bodi ya afya katika Halmashauri ya wilaya ya Tarime mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Apoo Tindwa anakemea viongozi wa bodi watakao kiuka agizo la serikali katika manunuzi ya dawa.

Nae mganga mkuu wa Hosipitali ya Halmashauri ya wilaya ya Tarime Hamidu Adinani alieza kwamba lengo la uundwaji wa bodi hizi za afya ni kuboresha huduma za afya kwa jamii.

Katika kikao hiki viongozi wa bodi za afya wametakiwa kuwa mstari wa mbele kujiunga na kuhimiza wananchi kujiunga na mifuko ya bima za afya ili kupunguza tatizo la kukosa matibabu katika vituo vya afya.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.