Chama cha wamiliki wa Mabasi ya abiria TABOA umekanusha kuwa hakutakua na mgomo wa kusafirisha abiria hapo kesho kama ilivyoripotiwa
Taharuki kubwa imezuka baada ya kusambaa kwa taaarifa ya Video ikitangaza mgomo wa nchi nzima kupinga Kanuni mpya za leseni.
Akizungumza Jijini Dsm Mwekahazina wa TABOA Issa Nkya amesema ni kweli wanapinga kanuni hiyo lakini hakuna mgomo bali kuna mgogoro wa kisheria na Sumatra.
Nkya amesema Jumatano ya November 15 kutakua na kikao na Sumatra kujadili kanuni na baada ya hapo tamko litatolewa.
Kwa upande Mkurugenzi wa huduma za Sheria kutoka Sumatra Tumaini Silaa amesema kanuni zinazolalamikiwa hazina tatizo lolote shida ni kwamba TABOA bado hawajizielewa.
Silaa amesema Kwenye mkutano wa Jumatano watawaelimisha wadau kuhusu kanuni hiyo, huku akitoa onyo kwa Mmiliki wa mabasi atakaethubutu kugoma.
Kanuni inayopigiwa kelele na TABOA ni ile inayosema kuwa dereva akifanya kosa, ataadhibiwa kwa kupelekwa Mahakamni na mmiliki wa basi hilo atatozwa faini.