Star Tv

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefutilia mbali azimio kuhusu vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Iran kuhusiana na suala la nyuklia. Azimio hilo lililowasilishwa na Marekani, lililenga kurefusha bila kikomo vikwazo vya silaha dhidi ya Iran.

Pendekezo jipya lililowasilishwa na Marekani linataka vikwazo hivyo kurefushwa bila ya kikomo ikisema iwapo vitaondolewa, Iran itakuwa msambazaji wa silaha bila kuzingatia maadili ya kimataifa.

Hata hivyo Marekani imetishia kurejesha vikwazo vilivyochukuliwa kabla ya kusainiwa kwa mkataba wa mwaka 2015.

Marekani imesema hatua hiyo itakomesha ufedhuli wa Jamhuri hiyo ya Kiislamu.

Marufuku iliyowekwa na Umoja wa Mataifa mwaka 2015 ya kuingiza au kuuza silaha zote za kivita kwa Iran inatarajiwa kufikia mwisho Oktoba 18 mwaka huu.

Rais wa Iran Hassan Rouhani alikuwa ameonya kuwa nchi yake ingejibu iwapo Baraza la Usalama lingerefusha vikwazo hivyo vya silaha lakini hakuainisha hatua watakazochukuwa.

Makubaliano ya nyuklia yaliyofikiwa kati ya Iran, Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Marekani yalianza kuyumbayumba baada ya Marekani kujitoa na Tehran kuanza

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.