Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani James Mattis amemshutumu Rais Donald Trump, kwa kuleta mgawanyiko na kutumia vibaya mamlaka yake.
Katika maoni aliyoyatoa Bwana Mattis amesema rais Trump ameamua kugawanya watu wa Marekani na pia ameshindwa kuonesha uongozi uliokomaa.
Anasema alikasirishwa na kufadhaishwa sana na jinsi Bwana Trump alivyoshughulikia maandamano ya hivi karibuni.
Tangu wakati huo amekuwa kimya hadi utawala wa Trump ulipokosolewa vikali katika gazeti la Atlanta Jumatano.
Bwana Mattis aliandika katika gazeti la The Atlantic..“Donald Trump ndio rais wa kwanza kwa maisha yangu ambaye hawaunganishi raia wa Marekani "Badala yake, anajitahidi kutugawanya, Tunashuhudia miaka mitatu ya hatua hizi za kukusudiwa na tunashuhudia matokeo ya miaka mitatu ya uongozi ambao haujakomaa.
Bwana Mattis pia alizungumzia wimbi la hivi sasa la maandamano dhidi ya ubaguzi wa rangi ambako kuchochewa na kifo cha raia Mmarekani mweusi George Floyd aliyekufa mikononi mwa polisi mapema mwezi huu.
Bwana Mattis alijiuzulu 2018 baada ya rais kuamua kuondoa majeshi ya Marekani kutoka Syria.