Star Tv

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Cote d'Ivoire na kiongozi wa zamani wa waasi Guillaume Soro amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na kosa la wizi pamoja na utakatishaji wa fedha.

Guillaume Soro ambaye yuko ukimbizini nchini Ufaransa, hakuwepo wakati hukumu hiyo ilipotolewa na mahakama ya Abidjan Jumanne wiki hii.

Guillaume Soro na wanasheria wake wanasema hukumu hiyo ilitolewa na mahakama baada ya kushinikizwa ili kumzuia kuwania nyadhifa ya uongozi nchini humo.

Hivi karibuni Guillaume Soro alitangaza kuwania katika uchaguzi wa urais ujao nchini humo uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Soro anashtumiwa kwamba alitumia fedha za umma takribani Euro Milioni Saba kujinunulia makaazi ya kifahari jijni Abidjan mwaka 2007 alipokuwa Waziri Mkuu.

Hata hivyo washirika wake wa karibu ikiwa ni pamoja na ndugu zake, wabunge na wafuasi wake wanaendelea kuzuiliwa nchini Cote d'Ivoire baada ya kukamatwa tangu mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka jana.

Kulingana na wanasheria hao, kesi hii ni ya kisiasa na ilianza kwa sababu Guillaume Soro, mshirika wa zamani wa Alassane Ouattara, aliachana naye na kutangaza kuwania katika uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.