Star Tv

Rais wa Marekani Donald Trump ameweka saini kwenye sheria ya inayositisha visa kwa wahamiaji kuingia nchini humo kwa siku sitini.

Hayo yanajiri wakati mipaka ya Marekani ambayo imefungwa kufuatia kuzuka kwa ugonjwa hatari unaotikisa dunia wa Covid-19.

Katika taarifa iliyotolewa na Ikulu ya White House ilieleza kuwa "Rais Trump amesitisha visa kwa wahamiaji ili wafanyakazi na raia wa Marekani wawe wa kwanza kunufaika ndani ya taifa lao na uchumi kufunguliwa tena".

Marekani ni miongoni mwa nchi ambayo imeathirika zaidi duniani na ugonjwa wa Covid-19, ambao mpaka sasa vifo vya watu zaidi ya 45,000 vimeripotiwa kutokana na ugonjwa huo.

Hatua ya kubaki nyumbani, imetajwa kuwaathiri kiuchumi Wamarekani milioni 22 baada ya kukosa ajira katika wiki za hivi karibuni.

Sheria hii ya rais Trump inahusu Visa za kudumu na haiwagusi wafanyakazi katika sekta ya afya, kwakuwa wafanyakazi hao wanaonekana kuwa ni muhimu.

Aidha, sheria hiyo iliyowekwa saini na rais Trump haiwagusi watu ambao tayari wako nchini Marekani ambao wanatafuta kibali cha kuruhusiwa kupata ajira ndani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.