Star Tv

Rais wa Marekani Donald Trump pamoja na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wamefunguliwa mashtaka ya kuhusika na jinai dhidi ya binadamu.

Raia kadhaa wa Marekani na Palestina wamefungua mashtaka dhidi ya viongozi wa Marekani na Israel ya 'kuunga mkono na kuhamasisha utendaji jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu' katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.

Kundi moja la raia wa Marekani na Palestina limewasilisha mashtaka hayo katika mahakama ya shirikisho ya Marekani dhidi ya Rais Donald Trump wa Marekani, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu pamoja na mkwe wa Trump Jared Kushner,.

Mashtaka hayo waliyofunguliwa ni kutokana na kile kinachojulikana kama  viongozi hao wanaunga mkono na kuhamasisha utendaji wa makossa ya jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina.

Raia hao wa Marekani na Palestina wamefungua mashtaka hayo katika kitengo cha mahakama ya shirikisho ya Marekani cha mji wa Columbia katika jimbo la Carolina ya Kusini.

Itakumbukwa kuwa tarehe 28 ya mwezi uliopita wa Januari Rais Donald Trump wa Marekani na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu walizindua mpango walioupendekeza wao wenyewe kuhusu Palestina walioupa jina la 'Muamala wa Karne'.

Mpango huo ujulikanao kama  wa 'Muamala wa Karne' vilevile unasemekana kuwa umeupuuza mpango wa mapatano wa Waarabu unaojulikana kama mpango wa Mfalme Abdullah pamoja na mapatano ya Oslo yaliyofikiwa kati ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina na utawala wa Israel.

                                                 Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.