Baraza la Seneti la Marekani limemuondolea hatia Rais Donald Trump na kuhitimisha mchakato wa mashtaka dhidi yake, ambapo wabunge wa chama cha Democratic walimtuhumu kutumia vibaya madaraka yake.
Wanachama wa chama cha Democrats walimshtaki Rais Trump mnamo mwezi Disemba na kushinikiza Ukraine kumtia mbaroni mpinzani wa White House.
Warepublican walio wengi katika baraza hilo walipata kura 52 ya kumuondoa hatiani Trump, dhidi ya kura 48 za upande uliounga mkono kumtimua katika wadhifa wake.
Baraza la Wawakilishi linaloongozwa na Kidemokrasia liliidhinisha nakala za mashtaka mnamo tarehe 18 Disemba.
Katika kura yake ya kihistoria Jumatano, Seneti iliamua kutomuondoa rais wa 45 wa Marekani madarakani kwa mashtaka yanayotokana na kushughulika kwake na Ukraine.
Wanachama wa chama cha democratic walihitaji theluthi mbili ya kura katika baraza hilo lenye wajumbe 100, ili kuweza kumtia hatia Rais Trump.
Kiongozi wa maseneta wa chama cha Democratic Chuck Schumer ameipuuza kura hiyo iliyomtakasa Trump akisema haina maana yoyote, kwa sababu Walipublican walikataa katakata kusikiliza mashahidi.
Rais Trump alikuwa akishutumia kwa kuomba msaada kwa serikali ya Ukraine kumsaidia achaguliwe tena mwezi Novemba,kusitisha kutoa misaada ya mamilioni ya fedha pamoja na msaada wa kijeshi kwa Ukraine mpaka rais wa nchi hiyo afanye uchunguzi dhidi mpinzani wake.
Aidha, hatua kadhaa zilipitiwa ili madai hayo kuitwa kesi ambapo mnamo Agosti 2019 watu walitoa madai dhidi ya rais Trump, Oktoba – Disemba uchunguzi ulifanyika , licha ya chama cha Trump kuwa na viti vingi zaidi ya wapinzani wake, mwezi Disemba kiongozi wa Democratic alipiga kura kumshtaki rais Trump na mwezi Januari 2020: Kesi ilifikishwa kwa seneti.
Mwisho.