Star Tv

Watu 176 wamepoteza maisha baada ya ndege ya abiria ya Ukraine kuanguka na kuteketea moto viungani mwa mji mkuu wa Iran, Tehran.

Msemaji wa Shirika la Usafiri wa Anga la Iran Reza Jafarzadeh, amesema  waliofariki dunia katika ajali hiyo ya alfajiri ya leo Jumatano katika eneo la Parand kaunti ya Robat Karim mkoani Tehran ni raia wa Iran.

Jafarzadeh amesema abiria wote 167 na wahudumu tisa wameaga dunia katika ajali hiyo, na kwamba ndege hiyo ilikuwa ikielekea katika mji mkuu wa Ukraine, Kiev.

Ali Khashani ambaye ni afisa wa ngazi za juu wa idara ya uhusiano mwema katika Uwanja wa Kimataifa wa Imam Khomeini mjini Tehran amesema, ndege hiyo aina ya Boeing 737 ya shirika la kimataifa la ndege la Ukraine UIA imeanguka muda mfupi baada ya kupaa angani kutoka uwanja huo, na kuteketea moto.

Kwa mujibu wa afisa huyo amesema huenda ajali hiyo imesababishwa na hitilafu za kiufundi lakini akasisitiza kuwa uchunguzi umeanzishwa ili kubaini kiini  cha ajali hiyo.

Afisa huyo wa Idara ya Uhusiano Mwema katika uwanja wa kimataifa wa Imam Khomeini mjini Tehran ameongeza kuwa ajali hiyo haijatatiza ratiba na safari zingine za ndege.

                                                                                             Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.