Star Tv

Vikosi vya polisi nchini Misri vimetawanywa kwa wingi katika eneo la kati la mji mkuu Cairo na kuzifunga njia zote za kuingia katika uwanja mashuhuri wa Tahriri, kufuatia wito wa maandamano dhidi ya rais Abdel Fattah al Sissi. Wito huo unafuatia tuhuma za rushwa ambazo rais Al Sissi anazikanusha.

Maandamano yameanza Septemba 20 mjini Cairo na katika miji mengine kadhaa kufuatia miito ya mtandaoni ya kuandamana kulaani rushwa katika familia ya al Sissi na jeshi lenye nguvu nchini humo. Rais al Sissi amerejea nyumbani akitokea New York, Marekani ambako alihudhuria Hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa. Akizungumza na umati wa watu waliofika uwanjani kumlahiki, rais al Sissi amewasihi wasitaharuki. Ameitaja risala iliyoenea mtandaoni na kumhusisha na rushwa kuwa ni uongo mtupu. Tangu maandamano ya mwishoni mwa wiki iliyopita kamata kamata inaendelea. Makundi yanayopigania haki za binaadam yanasema watu wasiopungua 2,000 wametiwa ndani hadi sasa.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.