Star Tv

Mji mmoja nchini Japan umetangaza onyo la dharura kuzuia watu kula samaki anayejulikana kama Fugu baada ya samaki huyo mwenye sumu kali kuuzwa kimakosa.

Maduka kwenye mji wa Gamagori yaliuza mifuko mitano ya Fugu bila ya kutoa maini yake ambayo yana sumu.

Mifuko mitatu imepatikana lakini mingine miwili bado haijapatikana.

Samaki huyo ana sumu na makosa kidogo yanaweza kusababisha maafa.

Mamlaka ya mji wa Gamagori kati kati mwa Japan imetoa tahadhari na kuwashauri watu kurejesha samaki hao.

Maini ya samaki huyo na ngozi huwa na sumu kali inayoitwa tetrodotoxin na mafunzo maalumu yanahiyajika pamoja na lesini kumuandaa samaki huyo.

Hakuna dawa ya kutibu sumu ya samaki huyo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.