Star Tv

Rais Donald Trump wa Marekani amefutilia mbali mpango wa kuzuru nchini Uingereza mnamo mwezi Februari ambapo alikuwa ametarajiwa kufungua ubalozi mpya wa taifa hilo uliogharimu takriban dola bilioni moja.

Katika ujumbe wake kwa Twitter, rais huyo wa Marekani alisema yeye sio shabiki wa ubalozi huo mpya ambao unahamia kutoka Mayfair kuelekea mjini London akidai kuwa ulikuwa ''mpango mbaya''.

''Jumba la zamani la ubalozi huo liliuzwa kwa fedha chache na utawala wa rais Obama'', aliongezea. Downing Street ilikataa kutoa tamko kuhusu hatua hiyo ya rais Trump.

Hatua hiyo ya ubalozi wa Marekani ilithibitishwa mnamo mwezi Oktoba 2008 wakati rais George W Bush alipokuwa mamlakani.

Hatahivyo rais Trump aliulaumu utawala wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Barrack Obama kwa kuuza eneo zuri la ubalozi huo kwa ''fedha chache''.

Alisema kuwa jengo hilo jipya katika eneo la Vauxhall, kusini mwa London lilikuwa katika eneo baya, akiongezea.''Walitaka mimi nilifungue rasmi-Hapana!''

Kwa hisani ya BBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.