Ubalozi wa Uingereza na Taasisi ya Mercy Corps pamoja na Chuo kikuu cha Dar es salaam kimetoa mafunzo ya namna gani ya kukabiliana na majanga mbalimbali yanayotokea katika jamii na namna ya kukabilina nayo ikiwa ni pamoja na mawasiliano pale dharura inapotokea.
Mratibu wa shirika la Mercy Corps Nchini Anthony Sarota wakati akitoa maelezo juu ya namna ya kukabiliana na majanga hayo amesema wameamua kutoa mafunzo hayo kwa Jeshi la Polisi ili kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia hasa kwa upande wa mawasiliano pale majanga yanapotokea.
Aidha kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP. Thabitha Makaranga ambaye pia ni mratibu wa mafunzo hayo kwa upande wa Jeshi la Polisi, amesema Jeshi hilo linashukuru wawezeshaji wa mafunzo hayo kwani yataleta tija na ufanisi wa kukabiliana na majanga ya dharura pindi yanapo tokea.
Kamishina wa Kamisheni ya Uchunguzi wa Kisayansi katika Jeshi la Polisi CP. Shaban Hiki akiongea katika hafla ya kufunga mafunzo hayo leo ambayo yamefanyika jijini Dar es salaam kuanzia Oktoba 10 hadi leo Oktoba 14, 2022 chini ya ufadhili wa ubalozi wa uingereza, taasisi ya mercy corps pamoja na wawezeshaji kutoka chuo kikuu dar es salaam amesema mafunzo hayo yatasaidia kuwajenga askari kiutendaji.