Star Tv
Mazishi ya Malkia Elizabeth II aliyekuwa kiongozi mkuu wa taifa la Uingereza ambaye alifariki Septemba 08, 2022 yatafanyika leo Septemba 19, 2022 jijini London nchini humo.
Mwili wake utasafirishwa kwanza hadi Westminster Abbey kwa ibada ya kidini mbele ya maelfu ya watu, na kisha kuelekea kasri la Windsor kwa ibada ya kifamilia na watu wa karibu zaidi, hatimaye, maziko ya kibinafsi.
 
Wakuu wa nchi kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni wamekuwa wakiwasili kuungana na washiriki wa familia ya Kifalme kukumbuka maisha na huduma ya Malkia.
 
Wanachama wa familia za kifalme kutoka kote Ulaya, ambao wengi wao walikuwa ndugu wa damu wa Malkia wanatarajiwa kushiriki katika mazishi hayo akiwemo Mfalme Philippe wa Ubelgiji na Malkia Mathilde, Mfalme Felipe wa Uhispania na Malkia Letizia.
 
Aidha pia viongozi mbalimbali kutoka Afrika tayari wamewasili akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.