Star Tv

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameamuru raia wote ambao bado wanaishi katika maeneo ya mashariki mwa mkoa wa Donetsk chini ya udhibiti wa Ukraine kuhama kutokana na kuongezeka kwa mapigano.

Eneo hilo limeshuhudia mapigano makali huku kukiwa na mwendo wa polepole wa vikosi vya Urusi kusonga mbele, ambavyo tayari vinadhibiti sehemu yake kubwa.

"Tutatumia fursa zote zinazopatikana kuokoa maisha ya watu wengi iwezekanavyo na kupunguza ugaidi unaotekelezwa na Urusi kadiri iwezekanavyo".

Kuingilia kati kwa Zelensky kunakuja wakati Urusi imewaalika maafisa wa Umoja wa Mataifa na Msalaba Mwekundu kuchunguza vifo vya wafungwa 50 wa vita wa Ukraine katika sehemu nyingine ya mkoa Donetsk.

Wakizungumza Jumamosi jioni, maafisa wa ulinzi wa Urusi walisema Moscow itakaribisha uchunguzi wenye "malengo’’ kuhusu tukio hilo na pia ilichapisha orodha ya kile ilichosema ni wafungwa wa kivita 50 waliouawa katika shambulio hilo.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.