Star Tv

Kaimu rais wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe ametangaza sheria ya hali ya hatari

Katika juhudi za kutuliza vurugu za umma na kuushughulikia uchumi ulioporomoka wa taifa hilo la kisiwa. Tangazo lililotolewa na serikali yake limesema ni sahihi kuchukua hatua kama hiyo kwa maslahi ya usalama wa watu, na kuhakikisha usambazaji wa mahitaji muhimu kwa jamii. Rais wa Sri Lanka aliyetimuliwa madarakani, Gotabaya Rajapaksa ambaye wiki iliyopita aliikimbia nchi, amesema alifanya kila awezalo kuepusha kusambaratika kwa uchumi wa taifa lake. Wickremesinghe ambaye alikuwa mshirika wa karibu wa Rajapaksa ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kuwania rasmi wadhifa wa rais, ingawa waandamanaji waliomfukuza mtangulizi wake wanataka yeye pia afungashe virago na kuondoka.

CHANZO: DW SWAHILI

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.