Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema taifa lake linahitaji silaha nyingi zaidi zitakazowasaidia kupambana na Urusi.
Katika hotuba yake ya kila Jumamosi, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesisitiza haja ya nchi yake kupatiwa silaha.
“Tunafanya kazi kila siku kuimarisha ulinzi wetu. Hii kimsingi ni kupata silaha, Bila shaka, kwa kiwango kikubwa inategemea na washirika wetu. Kwa utayari wao wakuipatia Ukraine kila kilicho muhimu kulinda uhuru wetu.”
Gazeti la New York Times limeripoti kwamba Ukraine “imepatiwa silaha na Denmark makombora ya Harpoon ya kujilinda na mashambulizi ya manowari za kivita,”.
Majeshi ya Urusi tayari yametangaza kuwa yameuchukua mji wa mashariki mwa Ukraine wa Lyman, kituo kikuu cha treni katika mkoa wa Donetsk. Kutekwa kwa mji huo kunaashiria mabadiliko ya kasi ya vita huko Ukraine.
Gavana wa mkoa Luhansk, ambao pamoja na Donetsk unaunda Donbas, alisema Ijumaa kuwa vikosi vya Urusi vimeingia Sievierodonetsk.