Star Tv

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema taifa lake linahitaji silaha nyingi zaidi zitakazowasaidia kupambana na Urusi.

Katika hotuba yake ya kila Jumamosi, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesisitiza haja ya nchi yake kupatiwa silaha.

“Tunafanya kazi kila siku kuimarisha ulinzi wetu. Hii kimsingi ni kupata silaha, Bila shaka, kwa kiwango kikubwa inategemea na washirika wetu. Kwa utayari wao wakuipatia Ukraine kila kilicho muhimu kulinda uhuru wetu.”

Gazeti la New York Times limeripoti kwamba Ukraine “imepatiwa silaha na Denmark makombora ya Harpoon ya kujilinda na mashambulizi ya manowari za kivita,”.

Majeshi ya Urusi tayari yametangaza kuwa yameuchukua mji wa mashariki mwa Ukraine wa Lyman, kituo kikuu cha treni katika mkoa wa Donetsk. Kutekwa kwa mji huo kunaashiria mabadiliko ya kasi ya vita huko Ukraine.

 

Gavana wa mkoa Luhansk, ambao pamoja na Donetsk unaunda Donbas, alisema Ijumaa kuwa vikosi vya Urusi vimeingia Sievierodonetsk.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.