Star Tv

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema taifa lake linahitaji silaha nyingi zaidi zitakazowasaidia kupambana na Urusi.

Katika hotuba yake ya kila Jumamosi, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesisitiza haja ya nchi yake kupatiwa silaha.

“Tunafanya kazi kila siku kuimarisha ulinzi wetu. Hii kimsingi ni kupata silaha, Bila shaka, kwa kiwango kikubwa inategemea na washirika wetu. Kwa utayari wao wakuipatia Ukraine kila kilicho muhimu kulinda uhuru wetu.”

Gazeti la New York Times limeripoti kwamba Ukraine “imepatiwa silaha na Denmark makombora ya Harpoon ya kujilinda na mashambulizi ya manowari za kivita,”.

Majeshi ya Urusi tayari yametangaza kuwa yameuchukua mji wa mashariki mwa Ukraine wa Lyman, kituo kikuu cha treni katika mkoa wa Donetsk. Kutekwa kwa mji huo kunaashiria mabadiliko ya kasi ya vita huko Ukraine.

 

Gavana wa mkoa Luhansk, ambao pamoja na Donetsk unaunda Donbas, alisema Ijumaa kuwa vikosi vya Urusi vimeingia Sievierodonetsk.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.