Star Tv

Rais wa Marekani Joe Biden alitia saini Sheria ya Kukodisha kwa Mkopo, iliyoundwa ili kurahisisha utaratibu wa kusambaza silaha kwa Ukraine.

Hati hivyo, kipengele hicho kilichopewa jina la "Sheria ya Kukodisha, Kulinda Demokrasia nchini Ukraine ya 2022," iliwasilishwa kwa Bunge la Congress hata kabla ya kuanza kwa uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, Januari mwaka huu.

Mnamo Mei 3, muswada huo uliidhinishwa kwa kura nyingi za Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani (417 waliunga mkono, 10 walipinga), na kabla ya hapo muswada huo uliidhinishwa na Seneti.

Kwa mujibu wa muswada huo, Rais wa Marekani "anaweza kuidhinisha serikali kukopesha au kukodisha mali ya ulinzi kwa Ukraine na nchi nyingine za Ulaya Mashariki zilizoathiriwa na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ili kusaidia kuimarisha ulinzi wa nchi hizi na kulinda raia dhidi ya mashambulizi yanayoweza kutokea au kuendelea".

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameishukuru Marekani na Biden kwa kufufua mpango wa msaada. "Asante @POTUS na watu wa Marekani kwa kuunga mkono Ukraine katika kupigania uhuru na mustakabali wetu," akaunti rasmi ya rais wa Ukraine ilituma ujumbe huo kupitia Twitter.

Wakati wa Vita vya Kidunia vya pili, mmoja wa wapokeaji wakuu wa misaada kama hiyo alikuwa Umoja wa Kisovieti.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alishukuru Marekani na Biden kwa kufufua mpango wa msaada. "Asante @POTUS na watu wa Marekani kwa kuunga mkono Ukraine katika kupigania uhuru na mustakabali wetu," akaunti rasmi ya rais wa Ukrain ilituma ujumbe huo kupitia Tiwtter kwa Kiingereza.

#ChanzoBBC

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.