Ukraine imesema inajiandaa kwa vita vya kemikali vinavyoweza kutokea kwa usaidizi wa taifa la Marekani.
Imeripotiwa kuwa Marekani imekuwa ikituma vifaa vya kinga (PPE) kwa Ukraine kwa ombi la nchi hiyo ili kujiandaa kwa shambulio lolote la silaha za kemikali wakati wa vita.
Msemaji wa Baraza la Usalama la Kitaifa la Rais Joe Biden amethibitisha kwamba "vifaa vya kuokoa maisha" vimetumwa.
Vifaa hivyo vya PPE vinadhaniwa kujumuisha barakoa za gesi, suti za hazmat na vifaa vingine.
Moscow na imekuwa ikirushiana tuhuma katika wiki za hivi karibuni kwamba silaha za kemikali na silaha za kibaiolojia zinaweza kutumwa.
Aidha, Maafisa wa Marekani wanahofia kuwa Urusi inaweza kuwa inapanga operesheni ya uongo ya bendera kuhusu matumizi ya silaha hizo.
#ChanzoBBC