Maafisa wa jeshi wa Ukraine wanasema wamefanikiwa kuziangusha ndege kadhaa za kijeshi za Urusi katika kipindi cha saa 24 zilizopita.
Maafisa hao wanataja ndege nne, helkopta 3 na zingine ndogo ambazo hazijatajwa zinazoonekana kuwa ni za jeshi la Urusi.
Ukraine inasema imeanza kufanya mashambulizi ya anga kwenye vituo vya kijeshi na maghala ya vifaa vya kijeshi vya Urusi, ili kuvuruga mifumo yake ya ysambazi silaha kwenye mpaka wa Ukraine.
Imeongeza kwamba vikosi vya Urusi havijaweza kusonga mbele, vikijielekeza zaidi kujiimarisha kaika maeneo ambayo tayari imesambaza majeshi yake.
Taarifa hiyo ya Ukraine inasema miundo mbinu ya kiaraia ikiwemo maeneo ya kuabudu yamekuwa yakiangaziwa na majeshi ya Urusi na kupeleka huko Silaha na vifaa vingine vya kijeshi.
Mpaka sasa BBC haijaweza kuthibitisha madai haya ya Ukraine.