Mkufunzi wa kibinafsi amefariki dunia baada ya kunywa kafeini ambayo ni sawa na vikombe 200 vya kahawa.
Baba wa watoto wawili Tom Mansfield alikuwa ametumia kimakosa kiasi cha unga alichotakiwa kutumia kwenye mizani ya jikoni.
Uchunguzi huko Ruthin umebaini kwamba kijana mwenye umri wa miaka 29 kutoka Colwyn Bay aliugua moja kwa moja baada ya kunywa mchanganyiko huo tarehe 5 Januari 2021.
Akifikia hitimisho la tukio hilo lisilo la kawaida, daktari wa John Gittins alisema chanzo cha kifo kilikuwa sumu ya kafeini.
Kafeini hutumiwa na baadhi ya washiriki wa mazoezi ya viungo, huku tovuti zingine za mazoezi ya mwili zikipendekeza kuwa unywaji wa kafeni kwa ajili ya kuboresha utendaji wa michezo katika viwango fulani.
Hata hivyo, wataalam wameonya kwamba wakati wa kunywa kafeni, kuna hatari ya kunywa zaidi ya kiasi kilichopendekezwa.
Siku ya Jumanne uchunguzi ulionesha Bw Mansfield alianza kufunga kifua na kulalamika moyo wake unapiga haraka baada ya kuteketeza bidhaa hiyo.
Dakika chache baada ya kwenda kujilala alianza kutokwa na povu mdomoni.
Mkewe Suzannah aliwaomba majirani na familia, na kuitisha ambulensi. Hapo ndipo wahudumu wa afya walipoanza kujaribu kumuamsha muda wa dakika 45 lakini baadaye alitangazwa kuwa amefariki katika Hospitali ya Glan Clwyd huko Bodelwyddan, Denbighshire.