Star Tv

Karibu watu 27,000 walilazimishwa kukimbia manyumba yao usiku wa manane wakati moto mkubwa ulisamba kwa haraka kusini kwa jimbo la Carlifonia.

Watu wamehamishwa kwa lazima kutoka makwao katika miji ya Ventura na Santa Paula karibu kilomita 115 Kaskazini mwa Los Angeles.Wazima moto walionya kuwa moto huo ulikuwa unasambaa kwa haraka na hawangeweza kuuzima.

Ukichochewa na upepo mkali moto uliosambaa ukubwa wa maelfu ya ekari kwa saa chache.

Gavana wa California Jerry Brown ametangaza hali ya tahadhari katika kaunti ya Ventura akiihaidi kukukabili moto huo kwa vyoyote vile.Mapema iliripotiwa kuwa mtu mmoja alifariki kwenye ajali ya barabarani akijaribu kuukimbia moto huo, lakini idara ya wazima moto kaunti ya Ventura imesema kuwa hakuna mtu aliyepatikana kwenye gari hilo lilikuwa limepinduka.

Maafisa walisema kuwa mzima moto alijeruhiwa. Pia walisema kwa nyumba 150 zilikuwa zimeharibiwa na watu 260,000 walikuwa hawana umeme.

Kwa hisani ya BBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.