Star Tv

Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte amesema anajiuzulu siasa na hatagombea katika uchauzi wa mwaka ujao.

Bwana Duterte mwenye umri wa miaka 76 mwezi uliopita amesema kuwa hatagombea kiti cha makamu wa rais mwaka 2022.

Katiba ya nchi hiyo inawaruhusu marais kuhudumu muhula mmoja wa miaka sita pekee.

Lakini sasa anasema ameamua kujiondoa kwenye uchaguzi wa mwaka ujao kwani "hisia za Wafilipino wengi ni kwamba sifai".

Hatua hii inakuja huku kukiwa na uvumi kwamba binti yake anaweza kugombea urais.

Bwana Duterte, mtu mwenye utata na "mwenye nguvu ", aliingia mamlakani mwaka 2016 ambapo aliahidi kupunguza uhalifu na kutatua mzozo wa madawa ya kulevya nchini humo.

Lakini wakosoaji wanasema katika kipindi cha miaka mitano akiwa mamlakani, Bw Duterte amewachochea polisi kufanya mauaji ya ukiukaji wa sheria ya washukiwa katika kile alichokiita "vita dhidi ya mihadarati ".

Mwezi uliopita Bi Duterte-Carpio alisema kuwa hatajiunga na kinyang'anyiro cha kuwania urais kwasababu yeye na baba yake wamekubaliana kuwa ni mmoja kati yao tu atakayegombea katika uchaguzi ujao utakaofanyika mwezi Mei.

Tangazo la ghafla la kujiuzulu kwa Bw Duterte Duterte amelitoa akiwa mjini Manila katika eneo ambalo alikuwa anatarajiwa kujisajili kama mgombea.

Alisema kuwa kugombea kama Makamu wa rais " kutakuwa ni kukiuka katiba ya nchi ".

Msemaji wake Harry Roque, hatahivyo, hakuelezea kwamba Bw Duterte ataondoka kabisa katika siasa katika siku zijazo.

Bw Roque ameiambia BBC kuwa tangazo hilo "linamaanisha kuwa hana haja na kuwa Makamu Wa rais na kuhusu iwapo atajiuzulu kabisa na kutoka katika siasa, nitahitaji kupata thibitisho la hili kutoka kwake".

Ana mtindo wa kusema mambo yanayofanana na hayo, na baadaye kugeuza usemi wiki moja baadaye.

Mwezi Septemba 2015, katika kampeni za kuelekea uchaguzi, aliyekuwa meya wa Davao wakati huo alisema alikuwa amepanga "kujiuzulu maisha ya umma daima ".

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.