Star Tv

Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanazingatia kutoa tamko la pamoja litakalohimiza kukomeshwa mara moja kwa mashambulizi ya kundi la Taliban nchini Afghanistan.

Rasimu ya tamko hilo iliyoshuhudiwa na shirika la habari la AP inaonya pia kwamba Baraza hilo halitaiunga mkono serikali yoyote itakayowekwa na nguvu za kijeshi ama kurudi kwa utawala wa Kiislamu wa Taliban uliokuwepo baina ya mwaka 1996 na 2001 nchini Afghanistan.

Tamko hilo ambalo ni la chini kuliko azimio, linatazamiwa pia kulaani mashambulizi ya Taliban dhidi ya miji mikubwa na midogo kote nchini Afghanistan.

Kwa mujibu wa nakala ya rasimu hiyo, Baraza la Usalama linaitaka serikali na kundi la Taliban kufanya mazungumzo yanayojumuisha makundi yote haraka iwezekanavyo na kufikia suluhisho la kisiasa la mgogoro wao.

Hayo yanajiri wakati Taliban ikiendelea kuchukuwa udhibiti wa majimbo, ambapo hadi sasa inahodhi majimbo 13 kati ya 34, likiwemo jimbo muhimu la Kandahar.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.