Star Tv

Mawaziri wa fedha kutoka kundi la mataifa 20 yaliyostawi na yanayoinukia kiuchumi kote ulimwenguni G20, wameidhinisha mkataba wa kihistoria wa kubadilisha mfumo wa kuyatoza ushuru mashirika ya kimataifa na kuzihimza nchi ambazo hazikushiriki kujiunga katika mkataba huo.

Mageuzi hayo yanayojumuisha ushuru wa kiwango cha chini cha asilimia 15 kwa mashirika ya kimataifa, yalikubaliwa na mataifa 131 mapema mwezi huu.

Lakini kuidhinishwa kwa mageuzi hayo na mataifa 19 yalioimarika zaidi kiuchumi pamoja na Umoja wa Ulaya kutasaidia kuhakikisha yanaanza kutekelezwa baada ya miaka mingi ya majadiliano.

Katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na mawaziri hao baada ya mkutano wa siku mbili ulioandaliwa mjini Venice na Italia inayoshikilia urais wa kundi hilo la G20, wamesema kuwa wamefikia makubaliano ya kihistoria kuhusu mfumo thabiti na bora zaidi utakaosimamia ushuru wa kimataifa.
#ChanzoDWSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.