Star Tv

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un amesema nchi yake inahitaji kujiandaa kwa mazungumzo na makabiliano na Marekani na haswa kujiandaa kikamilifu kwa mapambano.

Hii ni mara ya kwanza Bwana Kim kutoa maoni yake moja kwa moja juu ya utawala wa Rais Biden.

Korea Kaskazini ilikuwa imepuuza juhudi za serikali mpya ya Marekani kuanzisha mawasiliano ya kidiplomasia.

Bwana Kim alikuwa akizungumza kwenye mkutano wa viongozi wakuu huko Pyongyang.

Bwana Kim alisema wanahitaji kujiandaa kikamilifu kwa mapambano ili kulinda hadhi ya serikali yetu na masilahi yake kwa maendeleo huru, na vilevile kuhakikisha mazingira ya amani na usalama wa Korea Kaskazini, kulingana na chombo cha habari cha serikali KCNA.

Alisema pia Korea Kaskazini "kwa kasi na mara moja" itashughulikia maendeleo yoyote na "kuzingatia juhudi za kudhibiti hali kwa rasi ya Korea".

Maoni yake ya hivi karibuni yanakuja siku chache baada ya Bw. Kim kukiri rasmi kwamba Korea Kaskazini inakabiliwa na wasiwasi juu ya upungufu wa chakula.

Mnamo Aprili Bw. Biden aliitaja Korea Kaskazini kama tishio kubwa kwa usalama wa ulimwengu, na kusababisha jibu la hasira kutoka Korea Kaskazini ambayo ilisema taarifa hiyo ilidhihirisha dhamira ya Bwana Biden kuendelea kutekeleza sera ya uhasama kuelekea nchi hiyo.

Aidha, Washington pia hivi majuzi ilikamilisha ukaguzi wa sera yake ya Korea Kaskazini na kusema kuwa Marekani itaendelea kulenga hatimaye uharibifu kamili wa nyuklia katika peninsula ya Korea.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.