Star Tv

Idadi ya watu waliofariki kutokana na mfululizo wa milipuko katika kambi ya jeshi katika Jamhuri ya Guinea ya Ikweta imeongezeka na kufikia watu 98.

Maafisa wa wa Wizara ya Afya wanasema mlipuko huo ulitokana na silaha ambazo zilihifadhiwa vibaya ambayo ilichomeka baada ya moto uliowashwa na wakulima katika shamba lililokuwa karibu.

Idadi ya waliofariki iliongezeka baada ya wadumu wa kujitolea kuchukua karibi siku nzima kutafuta miili katika vifusi. Awali ilikadiriwa ni watu 31 pekee ndio waliofariki kutokana na mkasa huo.

Wizara hiyo imesema kuwa majeruhi 299 bado wako hospitalini wanaendelea kupata matibabu, Huku kundi la wataalamu wa afya ya kiakili pamoja na wauguzi wanaendelea kuwahudimia waathiriwa wa mkasa huo.

Karibu majengo yote na nyumba za makazi katika mji huo ziliharibiwa vibaya na mlipuko huo, Rais Teodoro Obiang Nguema alisema.

Katika taarifa, Rais Obiang Nguema alisema mlipuko huo ulisababishwa na uzembe uliohusishwa na hifadhi ya baruti kali katika kambi ya kijeshi ya Nkoantoma.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.