Star Tv

Baraza la Seneti la Marekani limefikia uamuzi kuwa kesi dhidi ya rais wa zamani wa nchi hiyo Donald Trump sio kinyume cha katiba.

Mawakili wa Trump walikuwa wamepinga vikali mchakato huo, kwa hoja kuwa ilikuwa ukiukaji wa katiba kumfungulia mashtaka rais ambaye hayuko tena mamlakani, akiwa na hadhi ya raia wa kawaida.

Kwa upande mwingine, maseneta wa Chama cha Democratic walisema kwamba hata ikiwa rais ameondoka madarakani, anapaswa kuwajibishwa kwa matendo aliyoyafanya akiwa ofisini.

Kupitia kura iliyopigwa jana jioni, maseneta sita kutoka chama cha Republican cha Trump walijiunga na Wademocrat wote 50, na kupitisha uamuzi huo kwa kura 56 dhidi ya 44 zilizopinga.

Katika mashtaka hayo ambayo ni ya pili dhidi ya Trump, kiongozi huyo anatuhumiwa kuchochea uasi katika majengo ya bunge mjini Washington mnamo Januari 6 mwaka huu, ambamo watu watano walipoteza maisha.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.