Star Tv

Saudi Arabia imetangaza kwamba mkutano wa nchi zilizostawi kiviwanda na kiuchumi (G20) utafanyika kwa njia ya video tarehe 21 na 22 Novemba mwaka huu.

Katika taarifa yake, Saudi Arabia, imesema mkutano huo utakuwa na kauli mbiu ya "Kuzipa uhalisia fursa za karne ya 21 kwa ajili ya wote".

Mkutano huo utakuwa kwa njia ya mtandao badala ya kukutana mjini Riyadh kama ilivyokuwa imepangwa mwanzoni

Kundi hilo la mataifa 20 linakusanya theluthi mbili ya idadi ya watu ulimwenguni, likiwa na asilimia 85 za uchumi na 75 ya biashara.

Mkutano wa kilele wa G20 huwaleta pamoja viongozi kutoka mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea ulimwenguni kuzungumzia ustawi wa maendeleo ya viwanda.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.